To Advertise on this Blog please Call: +255 (0)656 56 13 14 or Email: maishablog@yahoo.com                                                 To Advertise on this Blog please Call: +255 (0)656 56 13 14 or Email: maishablog@yahoo.com

Monday 4 July 2011

MSAADA TAFADHALI NDUGU WADAU.......


Mtanzania Mohamed Sakara aliyedhaniwa amekufa nchini Blugaria yu hai, anatafuta ndugu zake

Miezi michache iliyopita nilipokea barua pepe kutoka Bulgaria ikiniarifu kuwa kuna Mtanzania anaitwa Mohamed Sakara aliyedhaniwa amekufa lakini ilibainika kuwa yu hai na habari zake zikaandikwa kwenye gazeti moja la huko Bulgaria. 

Picha za hivi karibuni za Mohamed Sakara, akiwa jijini Sophia, nchini Bulgaria.
Raia wa Bulgaria aliyesoma hizo habari aliniandikia barua pepe kuniomba nijaribu kuwatafuta ndugu zake Sakara huku Tanzania. Nilituma hizo taarifa kwa mwanablogu Muhidini Michuzi lakini sina hakika kama zilitoka kwenye blogu yake.

Kwa kifupi Sakara alienda nchini Bulgaria kwenye miaka ya 1980 kusomea uhandisi, lakini hali ilimuendea vibaya mpaka kujikuta hana uwezo kabisa wa fedha na akiishi kwa shida mitaani. Angependa kurudi Tanzania lakini hana uwezo wa kujilipia nauli. Inasemekana baada ya kutangazwa amekufa, ndugu zake hawakuendelea kumtafuta, lakini ukweli ni kuwa yuko hai. Taarifa zake nyingine ni:
  • Amezaliwa mwaka 1961
  • Inakisiwa alisoma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kati ya mwaka 1982 - 1984 halafu akaenda Bulgaria ambako alikuwepo mpaka kipindi napata taarifa hizi
  • Anatoka kwenye familia ya watoto 8
  • Taarifa za kaka yake Abeid Hassan Sakara ni: amezaliwa mwaka 1954; ameandika kitabu "Jizoeze Kiswahili", na "Rashid Mfaume Kawawa"; alikuwa mkuu wa kitengo cha uchapishaji cha Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (Dar es Salaam); alikuwa akiishi Upanga Mashariki, Mtaa wa Maweni, Na.244, lakini hajulikani alipo kwa sasa.
Yoyote anayemfahamu Mohamed Sakara au ndugu zake awasiliane na mimi ili nimpe anwani ya aliyenitumia taarifa hizi toka Bulgaria.
source ;click here

No comments: