To Advertise on this Blog please Call: +255 (0)656 56 13 14 or Email: maishablog@yahoo.com                                                 To Advertise on this Blog please Call: +255 (0)656 56 13 14 or Email: maishablog@yahoo.com

Saturday 11 August 2012

Ajali nyingine Morogoro





Basi la kampuni ya Allys Sport Bus linalosafirisha abiria kutoka Dar es Salaam na Mwanza likiwa limeacha njia na kupinduka baada ya kutokea ajali inayodaiwa kusababishwa na basi la Shabiby lililokuwa likitokea mkoani Dodoma kwenda Dar es Salaam na kusababisha mabasi matatu kuacha njia katika eneo la Mkundi Makunganya barabaraba kuu Dodoma-Morogoro ambapo katika ajali hizo zaidi ya abiria 40 walijeruhiwa mkoani Morogoro



Mmoja wa majeruhi wa ajali ya basi la Shabiby, Deogratias Mrai akiwa katika wodi namba moja ya hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro akiuguza majeraha aliyopata kufuatia basi hilo walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kupinduka katika eneo la Mkundi-Makunganya Manispaa ya Morogoro lililokuwa likitoka Dodoma kwenda Dar es Salaam na kusababisha mabasi matatu kuacha njia katika eneo la Mkundi Makunganya barabaraba kuu Dodoma-Morogoro ambapo katika ajali hizo zaidi ya abiria 40 walijeruhiwa.

Na : Juma Mtanda

Kutoka Morogoro -- WATU 45 wamejeruhiwa kwenye ajali baada ya mabasi matatu waliyokuwa wakisafiria kuacha njia na kupinduka eneo la Mkundi kwa Makunganya nje kidogo ya Manispaa ya Morogoro, katika Barabara ya Morogoro - Dodoma.

Ajali hiyo ilitokea saa 2:30 asubuhi kwa kuhusisha mabasi matatu, Kampuni ya Shabiby lililokuwa likitokea Dodoma kwenda Dar es Salaam, Allys Sport na Sumry yaliyokuwa yakitokea Morogoro kwenda Mwanza.

Baadhi ya majeruhi waliokuwa wakisafiri na basi la Shabiby walisema basi hilo lilianza kuyumba na baadaye kuacha njia kisha kupinduka.

Mmoja wa abiria hao, Rashid Shaaban alisema baada ya basi hilo kupinduka, ghafla waliona basi jingine la Sumry likiacha njia na kupinduka wakati lilipojaribu kulipita gari jingine jirani na eneo hilo.

Alisema kuwa wakati kukiwa na msongamano wa magari katika eneo hilo la ajali, basi jingine la Allys Sport liliacha njia na kupinduka na hivyo kutokea ajali tatu katika muda usiozidi dakika 10.

Shaaban alisema baada ya ajali hizo walitokea watu waliokuwa wakijifanya kutaka kutoa msaada, lakini lengo lao lilikuwa ni kuiba mali za majeruhi. Hata hivyo, alisema lengo lao hilo halikufanikiwa kwani muda mfupi baada ya kutokea, askari walifika na kuimarisha ulinzi.

Katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, madaktari na wauguzi walionekana kuzidiwa na wagonjwa kutokana na idadi kubwa ya majeruhi waliokuwa wakihitaji huduma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile alithibitisha kutokea kwa ajali hizo na kusema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa zimetokana na utelezi na mwendo kasi.

Wednesday 8 August 2012

NDEREMO NA VIFIJO SIKU YA TAREHE 4/08/2012

 Mdau Raymond na Bibie Janeth wakiwa kanisani tayari kula viapo vyao vya ndoa hadi kifo kiwatenganishe...
 Hapa ni baada ya viapo na sasa ni mr and mrs Mkandawile
 Maharusi wakiteta jambo baada ya kunganishwa na kuwa mwili mmoja
 Bwana na bibi Harusi wakiwa nanyuso za furaha...
Maharusi na wapambe wao wakiwa kwenye picha ya pamoja

Friday 4 May 2012

Rais JK atangaza Baraza La Mawaziri.....


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Makamu wa Kwanza wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali na Waziri Mkuu Mh Mizengo Pinda baada ya kutangaza Baraza la Mawaziri leo April 4, 2012
(PICHA IKULU)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wanahabari wakati wa kutangaza Baraza la Mawaziri leo April 4, 2012
Wapiga picha wakiwa kazini wakati Rais Jakaya Kikwete akitangaza Baraza la Mawaziri leo ikulu
Wanahabari wakati Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa kutangaza Baraza la Mawaziri leo April 4, 2012
*************************
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898 
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
press@ikulu.go.tz 

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
ORODHA YA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI

MAWAZIRI

1. OFISI YA RAIS

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)
Ndugu Stephen M. Wasira, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)
Ndugu George Mkuchika, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)
Ndugu Celina Kombani, Mb.,

2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO)
Ndugu Samia H. Suluhu, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)
Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb.,

3. OFISI YA WAZIRI MKUU

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)
Ndugu Mary M. Nagu, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Hawa Ghasia, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)
Ndugu William V. Lukuvi, Mb.,

4. WIZARA

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Ndugu Samuel J. Sitta, Mb.,

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb.,

Waziri wa Ujenzi
Dr. John P. Magufuli, Mb.,

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb.,

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb.,

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Sophia M. Simba, Mb.,

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Bernard K. Membe, Mb.,

Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb.,

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb.,

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. David M. David, Mb.,

Waziri wa Kazi na Ajira
Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb.,
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof. Makame M. Mbarawa, Mb.,
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Prof. Anna K. Tibaijuka, Mb.,
Waziri wa Maji
Prof. Jumanne Maghembe, Mb.,

Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum
Prof. Mark Mwandosya, Mb.,
 
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Eng. Christopher Chiza, Mb.,
 
 Waziri wa Uchukuzi
Dr. Harrison Mwakyembe, Mb.,
 
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Dr. Fenella E. Mukangara, Mb.,
 
Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Khamis Kagasheki, Mb.,

Waziri wa Viwanda na Biashara
Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb.,

Waziri wa Fedha
Dr. William Mgimwa, Mb.,

Waziri wa Nishati na Madini
Prof. Sospeter Muhongo, Mb.,
 
5. NAIBU MAWAZIRI

OFISI YA RAIS
HAKUNA NAIBU WAZIRI

6. OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais
Ndugu Charles Kitwanga, Mb.,

7. OFISI YA WAZIRI MKUU
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb.,

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Aggrey Mwanry, Mb.,

8. WIZARA MBALIMBALI
Naibu Waziri wa Kazi na Ajira
Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb.,

Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Ndugu Adam Malima, Mb.,

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Pereira A. Silima, Mb.,

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
Ndugu Gregory G. Teu, Mb.,

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb.,

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb.,

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb.,

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb.,

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb.,

Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb.,

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Lazaro NyalanduMb.,
 
Naibu Waziri wa Ujenzi
Ndugu Gerson LwengeMb.,

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dr. Seif Suleiman RashidMb.,

Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Ndugu George Simbachawene, Mb.,

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Ndugu January Makamba, Mb.,

Naibu Waziri wa Uchukuzi
Dr. Charles J. Tizeba, Mb.,

Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Ndugu Amos Makala, Mb.,

Naibu Waziri wa Maji
Eng. Dr. Binilith MahengeMb.,

Naibu Waziri Nishati na Madini
Ndugu Stephen Maselle, Mb.,

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb.,

Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Janet Mbene, Mb.,

Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb.,

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
Mei, 2012

Wednesday 2 May 2012

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA YATANGAZWA..SHUKE ZA WAVULANA ZAFANYA VIZURI



 Baraza la Mtihani la Tanzania (Necta), limetangaza matokeo ya mitihani ya kidato cha sita iliyofanyika Februari mwaka huu yakionyesha kuongezeka kidogo kwa kiwango cha ufaulu kwa ujumla huku wavulana waliofaulu wakiwaacha mbali wasichana.

Katika matokeo hayo yaliyotangazwa jana na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), Dk Joyce Ndalichako (pichani), kati ya watahiniwa 46,499 waliofanya mtihani huo, wavulana waliofaulu ni 30,466 wakati wasichana ni 16,033. Hata hivyo, kumekuwa na mchuano mkali katika ufaulu kwa asilimia ambao wasichana walipata 87.37 na wavulana 87.69.

Sekondari ya Wasichana ya Marian, Bagamoyo ndiyo iliyoongoza kitaifa na mwanafunzi wake, Faith Assenga ndiye aliyeshika namba moja katika masomo ya Sayansi.

“Katika masomo ya Biashara, aliyeshika nafasi ya kwanza ni Alex Isdor wa Sekondari ya Kibaha na Lugha ni Faridi Abdallah wa Sekondari ya Mpwapwa,” alisema Dk Ndalichako.

Dk Ndalichako alisema kiwango cha kufaulu kwa watahiniwa 46,499; wakiwemo wale wa kujitegemea, kimeongezeka kutoka asilimia 87.24 mwaka jana hadi 87.58 mwaka huu.

Hata hivyo, alisema mwaka huu watahiniwa wa shule wameanguka katika masomo ya kemia, hisabati ya msingi, uchumi na maarifa ikilinganishwa na mwaka jana.

“Masomo ambayo wanafunzi walifanya vizuri zaidi ni Historia, Jiografia, Kiswahili, Kiingereza, Fizikia, Elimu ya Mimea, Biashara, Uhasibu na Hisabati daraja la juu," alisema.

Shule Bora

Dk Ndalichako alisema Necta imezigawa shule zilizofanya vizuri katika makundi mawili; zenye watahiniwa zaidi ya 30 na zenye watahiniwa chini ya 30.

“Kwa shule zenye watahiniwa 30 au zaidi, sekondari 10 zilizofanya vizuri zaidi ni Marian (wasichana) ikifuatiwa na Feza (wavulana), Kisimiri, Kibaha, Ilboru, Mzumbe, Msalato, Tabora (wavulana), St. Mary's Mazinde Juu na Consolata Seminari.

Sekondari zilizofanya vibaya zaidi katika kundi la shule hizo ni Pemba Islamic, Zanzibar Commecial, Kongwa, Uweleni, Mazizini, Lumumba, Ben Bela, Mlima Mbeya, Laurate International na Haile Selassie.

Sekondari iliyoongoza kwa kufaulu katika kundi la shule zenye watahiniwa chini ya 30 ni Uru Seminari ikifuatiwa na Iwawa, Maua Seminari, Harrison Uwata, Beroya, Palloti, Lutengano, Makita, Mwanga na Visitation (wasichana).

Sekondari zilizofanya vibaya zaidi kwenye kundi hilo ni Mbarali Preparatory, Philter Federal International, High-View International, Kifai Modern, Sha, Dar es Salaam Prime, Kandoto Sayansi, Popatlal, Al-Falaah Muslim na Kiuma.

Wanafunzi bora

Dk Ndalichako alisema mwaka huu walishindanisha ubora wa watahiniwa kwa kuzingatia aina ya masomo wanayochukua.

Katika kundi la wanafunzi bora kwenye Sayansi lililoongoza na Faith, aliyefuata ni Zawadi Mdoe (Feza), Belnadino Mgimba (Minaki), Jamal Juma (Feza) na Imaculate Mosha (Marian).

Watano waliofanya vizuri katika masomo ya Biashara wakiongozwa na Alex ni Ephraim Tumwidike (St Joseph's Cathedral), Vaileth Mussa (Weruweru), Seleman Manyiwa (Kibaha) na Hussein Issa (Azania).

Katika masomo ya Lugha na Sayansi ya Jamii aliyemfuata Faridi ni Jema Rwihura (Weruweru), Mariam Hincha (Weruweru), Neema Mbandwa (Igawilo) na Hemed Hussein (Tosamaganga).

Wasichana watano bora kwa masomo ya Sayansi, wote wametoka Marian ambao ni Faith Immaculate Mosha, Rachel Sigwejo, Mary Kiangi na Nashival Kivuyo.

Wavulana bora katika Sayansi ni Zawadi, Belnadino, Jamal Juma (Feza), Gwamaka Njobelo na Nickson Mwamsojo; wote kutoka Mzumbe.

Wasichana waliofanya vizuri zaidi katika masomo ya Biashara, nafasi ya kwanza hadi ya nne ilichukuliwa na wanafunzi wa Weruweru, ambao ni Vaileth, Gloria Murro, Stella Richard na Helen Komba. Nafasi ya tano ilichukuliwa na Veronica Sauli wa St. Antony.

Wavulana waliofanya vizuri katika masomo ya biashara ni Alex, Aphraim, Suleiman, Hussein na Ally Katala wa Azania.

Wasichana watano waliofanya vizuri masomo ya Lugha na Sayansi ya Jamii ni Jema, Mariam, Neema Mbandwa (Igawila), Angel Ruhumbika (Loreto) na Jaquline Chambua (St. Mary's Mazinde Juu).

Wavulana waliofanya vizuri katika masomo ya Lugha na Sayansi ya Jamii ni Faridi, Hemed, Elibaraka Mmari (Lyamongo) na Salvatory Kessy (Majengo).

Matokeo yaliyozuiwa

Dk Ndalichako alisema watahiniwa sita, watatu kati yao wakiwa wa kujitegemea walifutiwa matokeo yao baada ya kubainika kuwa walifanya udanganyifu.

Alisema pia Necta imezuia matokeo ya watahiniwa 51 ambao kwa mujibu wa kumbukumbu zao hawajalipa ada ya mtihani.Dk Ndalichako alisema matokeo yao yatatolewa na Necta pindi watakapokamilisha taratibu za malipo hayo.

Sekondari 10 Bora
1. Marian (wasichana) - Pwani
2. Feza (wavulana) - Dar es Salaam
3. Kisimiri - Arusha
4. Kibaha - Pwani
5. Ilboru - Arusha
6. Mzumbe - Morogoro
7. Msalato - Dodoma
8. Tabora (wavulana) - Tabora
9. St. Mary's Mazinde Juu - Tanga
10. Consolata Seminari - Iringa

Wanafunzi 5 bora Sayansi

1. Faith Assenga - Marian
2. Zawadi Mdoe - Feza
3. Belnadino Mgimba - Minaki
4. Jamal Juma - Feza
5.Imaculate Mosha - Marian

Wanafunzi 5 bora biashara

1. Alex Isdor -Kibaha
2. Ephraim Tumwidike - St Joseph's Cathedral
3. Vaileth Mussa -Weruweru
4. Seleman Manyiwa -Kibaha
5. Hussein Issa - Azania

5 bora Lugha na Sayansi ya Jamii

1. Faridi Abdalla - Mpwapwa
2. Jema Rwihura - Weruweru
3. Mariam Hincha - Weruweru
4. Neema Mbandwa - Igawilo
5. Hemed Hussein - Tosamaganga
                                          kwa matokeo ya jumla Angalia hapa

Tuesday 1 May 2012

Hotuba Ya JK Tanga Na Furaha Ya Rais; Tafsiri Yangu



Ndugu zangu,

Mwaka huu nilipata kumfundisha mwanahabari kijana namna ya kufungua blogu. Nikamwelekeza kwa kutumia mfano, namna ya kuweka picha kwenye blogu yake mpya niliyomsaidia kujifunza namna ya kuifungua. Nikachagua picha ya mwanasiasa kijana wa CCM, nikaiweka kwenye blogu yake.

Nilipomaliza, akaniomba haraka sana nimfundishe namna ya kuondoa picha kwenye blogu yake. Hakutaka kabisa picha hiyo ya mwanasiasa kijana wa CCM ikae kwa muda mrefu kwenye blogu yake. Akanitamkia; kwa kweli sitaki kabisa kuwaona hawa jamaa kwenye blogu yangu.

Kiukweli, vijana wengi kwa sasa  wanaichukia CCM, na labda zaidi, wanauchukia ufisadi, na wanawachukia viongozi mafisadi na  ambao wanaamini wanalelewa na wanalindwa na CCM. Ndio maana ya vijana wengi leo kuchukia chochote kile kinachohusu CCM, ikiwamo rangi ya kijani.

Jana usiku nilisikiliza kipindi maalum TBC1 kilichorusha hotuba ya JK ya Mei Mosi aliyoitoa Tanga.
Tafsiri yangu;

Hakika, ni moja ya hotuba bora za JK alizopata kuwahutubia Watanzania.
 Ni yenye kutoa matumaini kwa wengi na yenye kuwasuta wanafiki wachache walio ndani ya chama chake. JK akiendelea kwa staili ile, basi, anaweza kuanza kuibadili mitazamo ya wengi juu yake, mitazamo ambayo kwa sasa mingi ni hasi.

Na JK akatamka, kuwa yale ya Dodoma  ( Bungeni) hayakumsikitisha wala kumfadhaisha, badala yake yamemfurahisha. Yumkini JK anajihisi kuanza kuutua mzigo. Lakini, furaha yake yaweza kuwa ya muda mfupi kama asipokwenda, kwa vitendo, mbali zaidi na kushiriki kazi ya kweli ya kuwakomboa Watanzania kutoka kwenye hali ya sasa ikiwamo kudhalilishwa hata kwa kuhongwa pilau kwenye chaguzi kutokana na njaa zinazotokana na  viongozi na watendaji ' mapanya' wanaotafuna mali ya umma.

Nilimwona jana, JK anayejiweka mbali na ’ madudu’ yaliyoainishwa na CAG na yaliyowafanya baadhi ya wabunge wakiwamo wa CCM wachachamae Bungeni na hata kufikia hatua ya kuweka saini zao kushinikiza mawaziri wajiuzuru.
JK alichowaambia Watanzania jana ni kuwa yuko pamoja nao kwenye kilio chao cha ufisadi uliokubuhu  na unaofanywa na viongozi na watendaji waliopewa dhamana ya kulinda rasilimali za umma.

JK anasema- Kule kwenye halmashauri fedha zinatafunwa utadhani hazina mwenyewe! Ametumia lugha ya mtu wa kawaida na kwa kweli hicho ndicho ambacho umma umekifahamu kwa siku nyingi na Chadema ndio imeonekana kuwa mtetezi wao anayewasaidia kupambana na wezi wao. Hivyo basi, ni moja ya sababu ya kuongezeka kwa umaarufu wa Chadema na kupungua kwa kasi, umaarufu wa CCM. Maana, Chadema sasa ndio inaonekana kuwa ni kimbilio la wanyonge.

Kwa hotuba ile ya jana, JK ana fursa njema sasa ya kujiwekea legacy. Yale ya kukumbukwa nayo hata baada ya kuondoka madarakani; kusimama upande wa umma na kushiriki kwa vitendo kuwaandama viongozi na watendaji waliojigeuza miungu watu na huku wakishiriki wizi wa mali ya umma.  Na wengi wao wamo ndani ya CCM, au wanalindwa na CCM, Chama tawala.

Maana, 
wahenga  walinena; kila jambo lina dalili. Na nimepata kuandika, kuwa Afrika mvua hainyeshi ghafla, huanza na  mawingu kujikusanya. Ndio maana ya umuhimu wa kusoma alama za nyakati. Na kwenye nyumba panya huanza na shimo moja. Na mashimo ya panya yakiongezeka, basi, mwenye nyumba huwa na  kazi ngumu kupambana na panya hao.


Na huko nyuma nimepata kuandika, kuwa kuna wachache ndani ya CCM ambao Chama wamekigeuza kuwa ’ Shimo la Panya’- watoke wakatafune mali ya wananchi, kisha wakimbilie shimoni kwa maana ya kwenye chama. Na shimoni ndiko kwenye ’ kulindana’. Na hii ndio sababu ya msingi ya kupungua umaarufu kwa chama hicho tawala miongoni mwa Watanzania na hususan kundi kubwa la vijana.

Maana, ni ukweli, wengi wanaotuhumiwa kushiriki  ufisadi wamo ndani ya Chama tawala . Ni  wenye  mahusiano mazuri au kama inavyosemwa siku hizi, ni ’ marafiki’ wa CCM. Naam , hivi ni vijipanya tu  ni vyenye  ’vijishimo vyao’  ndani ya CCM. Si tumepata kusikia ikitamkwa; ” Ukitaka biashara yako ikunyokee, njoo CCM!”

JK wa sasa anaweza kuweka historia kwa kuongoza kazi ya kuondokana na ubaguzi wa kisiasa katika nchi yetu.  Ubaguzi huu wa mathalan, ’ Hawa ni wenzetu’ na ’ Wale ni maadui zetu’ umejengeka katika misingi ya kulindana katika maovu.  Wenye kuendekeza ubaguzi huu  ndio wenye kugombania fito wakati tunajenga nyumba moja.  

Jeffrey Sachs ni Mwanauchumi maarufu na ambaye JK amepata kukutana na kuongea naye kwenye Ikulu yake. Profesa Jeffrey Sachs ana mfano hai wa Poland.  Katika kuwashauri  kuinuka kiuchumi WaPoland wale , Profesa Sachs aliwaambia; ” Political power must be shared”.  Kwamba kuna umuhimu wa vyama kuwa na utayari wa kugawana madaraka ya uongozi wa kisiasa.

Ndio, Fundi Umeme yule Lech Walensa wa chama cha wafanyakazi na aliyeanzisha vuguvugu la mapinduzi ya kujikomboa kutoka Ukomunisti nchini Poland aliambiwa na Profesa Jeffrey Sachs; ”  Chama chako cha Solidarity kiwe radhi kuunda Serikali ya Mseto na Chama Cha Kikomunisti”. Na ikawa hivyo, kimoja kikatoa Waziri Mkuu na kingine Rais.  Kukawepo utulivu wa kisiasa. Poland ikaanza kupiga hatua za maendeleo ya kiuchumi. Ndio, hakuna uchumi unaokua bila uwepo wa utulivu wa kisiasa.

Maana tunakumbuka siku ile JK alipotangaza mpango wa kiuchumi wa miaka mitano kule Dodoma, JK alitamka;  " Bila Utawala Bora , bila kuwa na demokrasia, bila kuheshimu Haki za Kibinadamu,  mafanikio ya kiuchumi hayatawezekana."

Rais  hakupigiwa makofi  ya nguvu. Ndio, wengi wa viongozi waliokuwa wakimsikiliza JK kwenye ukumbi ule wa Saint Gasper pale Dodoma ni Wana-CCM. Bila shaka kuna waliokuwa wakifikiria Ukuu wa Wilaya wao na Ukuu wao wa Mkoa. Walifikiria nyadhifa  zao. Mambo ya kupanua demokrasia ikiwamo uwepo wa  vyama vingi  kwao ina tafsiri ya kutishia vibarua vyao!

Nimepata kuandika;  kama kwenye nyumba yako umeingiliwa na panya wanaotafuna  vyakula na hata akiba yako ya nafaka, basi, mwenye nyumba una mawili ya kufanya; kusalimu amri na kuwaacha panya hao watafune mpaka nguo unazovaa au kuchukua hatua ya kupambana na panya hao.  Na kama panya ni wengi dawa ni kuitafuta sumu ya panya.

 Na nchi ni hivyo hivyo, swali ni hili; tunafanyanye , pale panya wachache,  kwa kutumia chama cha siasa kama shimo la kujifichia tunawaona  wakitafuna  mali za  wananchi usiku na mchana?

 Jibu; KATIBA MPYA ndio ’Sumu ya panya ’ tunayoihitaji  sasa kupambana na panya wachache wanaoitafuna nchi yetu. Panya hawa wakijua kuwa kuna Jaji wa Mahakama ambaye hakuchaguliwa na Rais wa chama chao bali kaidhinishwa na Bunge la wananchi, basi, wataogopa hata kuiba kalamu za ofisini.  Ndio, mengine yote nje ya kukaa chini kama taifa na kuandaa Katiba Mpya itakayotokana na wananchi ni  sawa na kutwanga maji kwenye kinu. 


Maggid Mjengwa,
Msamvu, Morogoro
0788 111 765

Monday 30 April 2012

SOMA PATA DEGREE YA UK NCHINI MALAYSIA KWA GHARAMA NAFUU

LOCAL ADDRESS

HAIDERY PLAZA
FIRST FLOOR T-16
KISUTU/UPANGA STREET
DAR ES SALAAM
TANZANIA
CONTACT NUMBERS 0716623656 OR 0713586614
EMAIL: ally.abdallah@lsclondon.co.uk 

Friday 27 April 2012

RAY ANENA JUU YA KIFO CHA SWAIBA WAKE KANUMBA..



Ikiwa ni tariban mwezi sasa umepita tangu msanii maarufu wa filamu, Steven Charles Kanumba afariki dunia, msanii mwenzake Vincent Kigosi ‘Ray’ ameamua kuandika waraka mzito kueleza kwa nini hahusiki na kifo cha swahiba wake huyo kama ambavyo imekuwa ikisambazwa na watu wasiomtakia mema.

Waraka huo ulinaswa hivi karibuni kupitia blogu yake ambapo baada ya timu ya gazeti hili kuupitia ikaona ni vyema ukasomwa na Watanzania wote ili kuweza kupata jibu la kwa nini yeye hahusiki? Waraka huo ni huu hapa chini…

******************

Yapata wiki tatu sasa tangu msanii mwenzangu Steven Kanumba aage dunia na kama ilivyo kwa kila kitu kinapotokea huandamana na kila aina ya maneno na hisia mbalimbali kutokana na mitazamo ya watu kupishana kuhusiana na jambo husika. 

Kulingana na muktadha huo, msiba wa Steven Kanumba umekumbwa na maneno na hisia kama hizo, hususan mazingira ya kifo chake. Kinachosikitisha zaidi watu wengi (ambao wanajitambulisha kama wapenzi wa Kanumba) na baadhi ya vyombo binafsi vya habari vimekuwa vikinihusisha na kifo hicho kwa kusema kwamba kwa njia moja au nyingine nahusika na mauaji ya Steven Kanumba. 

Kwa muda wote huo tangu msiba ulipotokea mpaka leo hii nashika kalamu kujaribu kuyaweka sawa na kuondosha hisia chafu katika fikra za watu. Nimekuwa nikipitia katika wakati mgumu sana kwa jinsi ambavyo nimekuwa nikinyooshewa vidole kila upande nikihusishwa na kifo hicho.

Kiujumla nimezingatia maoni ya wapenzi na mashabiki wangu wakinitaka kuwa na subira ila kuna usemi usemao, uongo ukirudiwa sana jamii huusadiki na kuuona ukweli, nimeona nisikae kimya ila niweke sawa hili kwamba sihusiki na kifo cha Steven Kanumba.
Nasema wazi kwanza sihusiki kabisa na kifo cha Kanumba kwa kuzingatia mazingira yenyewe ya kifo kilivyotokea. Wakati kifo hicho kinatokea, nilikuwa sehemu nyingine kabisa na mimi nilikuwa mtu wa tatu kutaarifiwa kwamba Kanumba amepatwa na mkasa ambao baadaye ulisababisha kifo chake. 
Hata nilipofika katika Hospitali ya Muhimbili (tofauti na watu wanavyodhani kuwa nilifika nyumbani kwake, ukweli mimi nilimkuta tayari amepelekwa Muhimbili), nilikuta tayari alikuwa ameshafariki ndiyo maana hata polisi wanaohusika na usalama wa raia, si tu kwamba hawakuniweka chini ya ulinzi, sikuitwa hata kuhojiwa kwa sababu hakuna mazingira yoyote yanayonihusisha mimi na kifo hicho.
Pengine watu wanaojaribu kuongea hayo, hawajui mimi na Steven Kanumba tumetoka wapi? Sisi si watu tuliokutana barabarani, tuna historia katika kazi yetu ya sanaa na pia katika maisha  yetu. Mwanzoni kabisa, mimi ndiye niliyempokea Kanumba pale Kaole na ndiye niliyemfundisha sanaa pale (nadhani watu wanakumbuka tamthiliya za wakati huo ITV).
Baada ya hapo tulienda pamoja katika Kampuni ya Game 1st Quality na tukafanya filamu kama Johari, Sikitiko Langu, Dangerous Disire na nyinginezo na tuliendelea kuwa pamoja katika kampuni hiyo mpaka tulipofanya filamu ya Oprah mwaka 2008 ambapo niliingia rasmi kufanya kazi za kampuni yangu, lakini tuliendelea kuwa pamoja hata wakati nikiendelea na kazi za kampuni yangu. 
Pia mimi nilikuwa wa kwanza kuanza kufanya kazi na Steps na baadaye Kanumba alipoanza kufanya kazi zake mwenyewe na kunikuta huko tuliendelea kuwa pamoja kama siku zote. Kitu kikubwa kilichokuwa kinaendelea baina yetu ni kwamba tulijenga ushindani wa kuendeleza kazi mbele kwa kila mmoja akitoa kazi, mwingine anamjibu.
 Isitoshe hata vitu vyetu binafsi utaona kama kuna kufanana. Kuna wakati Kanumba alinunua Toyota Rav 4 nyeusi mimi nikanunua ya kijani, aliponunua Harrier na mimi nikanunua pia na hata gari za hivi karibuni, ukitazama utaona kuwa zinafana kwa karibu. Hii ilikuwa ni kama maisha yetu, hatukuwa na uadui, ilikuwa tunapeana changamoto za maendeleo.

Watu wanaojaribu kuonesha kuwa tofauti zetu ilikuwa ni uadui, huwa hawajui wapi tulikotoka ndiyo maana wanasema wasemavyo na katika kuthibitisha kuwa tofauti hizo hazikufikia katika uadui, kuna watu ambao wanafanya kazi nami katika kampuni yangu ya RJ ndiyo hao hao Kanumba alikuwa anawatumia siku zote katika kazi zake, hata baada ya tofauti hizo hakuna aliyekoma kufanya kazi na yeyote kati yetu. 

Kumtuhumu mtu kwa namna yoyote ile bila ya uthibitisho wa tuhuma hizo, ni kosa kwa sheria za nchi na pia kama ni mfuasi wa dini yoyote ni dhambi, kwani wakati ukisema hayo huku hujui uhalisia bali unasukumwa na nguvu za hisia tu ni sawa na kumchafua mtu huyo katika jamii bila ya kujua jamii inamchukuliaje.

Napenda kusema wazi kuwa, kwa kila anayetekwa na wimbi hili, ajaribu kufikiria leo ipo kwangu mimi, kesho inaweza kuhamia kwako, kwani mimi siyo wa kwanza kufikwa na haya. Inaweza kukukuta hata wewe au ndugu yako, utajisikiaje!

Na kama kweli mimi nimehusika na kifo cha Kanumba kwa namna yoyote ile, basi Mungu atanihukumu na kila aliye hai atashuhudia ila kama sijahusika kwa lolote, Mungu hatonihukumu na badala yake ataniinua kwa kuwa ninapita katika kipindi kigumu mno sasa hivi kwa madhira haya.

Mwisho kabisa napenda kumaliza kwa msemo usemao, ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke kwani kadiri mambo haya yanavyoendelea, usidhani yataishia kwangu, kwani mkono wa dhuluma hauishii karibu, ukisikia jirani anapiga kelele za mwizi, usilale nenda kamsaidie.

Usiseme kuwa hatuhusiki kwani hayupo kwetu, kesho utafikwa na wewe utakosa wa kukusaidia. Cha msingi kama tunampenda sana ndugu yetu ni kumuombea kwa Mungu, kwani hatujui makao yake huko aliko na siyo kuunda vitu ambavyo kamwe hata yeye angekuwa hai asingeviafiki.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU STEVEN KANUMBA MAHALI PEMA

PEPONI -AMINA.