To Advertise on this Blog please Call: +255 (0)656 56 13 14 or Email: maishablog@yahoo.com                                                 To Advertise on this Blog please Call: +255 (0)656 56 13 14 or Email: maishablog@yahoo.com

Saturday 15 January 2011

MAHUJAJI ZAIDI YA 100 WAFA AJALINI NCHINI INDIA!!

Habari kutika nchini India zinasema zaidi ya mahujaji 100 wamekufa kwa ajali wakati wakiwa njiani kutokea kwenye ibada yao ya hija maeneo ya milimani kusini mwa jimbo la Keral.
Chanzo cha ajali hiyo kinasemakena kuwa ni kupoteza mwelekeo kwa gari aina ya jeep iliyokuwa imejaza watu ndani yake na hivyo kuseleleka na kuwaangukia mahujaji hao. Kwa mujibu wa taarifa za polisi wamesibitisha kuwa vifo vingi vilisababishwa na mshituko na hivyo kukanyagana na kukosa hewa.Hii ni mara ya pili sasa kutokea kwa majanga katika eneo hilo kwani mwaka 1999 watu zaidi ya 50 walipoteza maisha kutokana na kuporomoka kwa udongo na kuwafunika mahujaji.
Eneo hilo maarufu la sala hutembelewa na watu zaidi ya millioni tatu kila mwaka.



No comments: