To Advertise on this Blog please Call: +255 (0)656 56 13 14 or Email: maishablog@yahoo.com                                                 To Advertise on this Blog please Call: +255 (0)656 56 13 14 or Email: maishablog@yahoo.com

Saturday 15 January 2011

VURUGU BADO ZARINDIMA UDOM,MKUU WA MKOA NA WILAYA WATEKWA NA WANAFUNZI.........WADAI PROF.MLACHA AJIUZURU..

copyright;maisha blog

Sehenu ya umati wa wanafuzi wakiwa kwenye maandamano UDOM
Habari zilizotufikia mezani jioni hii kutoka katika chuo kkuu cha Dodoma (UDOM) zinathibitisha kuwa mkuu mkoa na wa wilaya ya Dodoma wametekwa na msafara wake na wanafunzi wa chuo cha elimu UDOM, wanafunzi hao walikuwa wakimtaka waziri mkuu Mh. Mizengo Pinda aje na kumuondoa makamu mkuu wa chuo fedha na utawala Prof.Mlacha.
Wakionekana kuwa  wenye hasira walitoa upepo kwenye rairi za gari za wakuu hao pia kuziba vioo vya gari kwa mabango ili kuzuia msafara huo usiondoke hadi pale Waziri mkuu atakapo toa tamko la kumuondoa Prof. Mlacha ambaye wanaona ndiye kikwazo chuoni hapo.
vijana hao wakiwa wamecharuka kabisa, wanataka mkuu huyo wa fedha mipango na utawala asiendelee na nafasi yake kwani anadharau na majibu ya kejeli kwa wanafunzi na wahadhiri wa UDOM. Akisoma taarifa kwa waziri mkuu, kiongozi wa wanafunzi alimshambulia sana DVC PFA huyo prof. Mlacha na kumtaka kuachia madaraka mara moja ili kupisha maendeleo chuoni hapo.
Waziri mkuu alikitembelea chuo hicho cha Dodoma (UDOM) leo na kuzungukia maeneo mbalimbali chuoni hapo kisha kuahidi kurudi kuongea na baadhi ya makundi kadhaa ya wana UDOM hususani Wanataaluma ambao wapo kwenye mgomo baridi tangu J3 manamo saa saba mchana lakini hakuweza kurudi chuoni hapo na badala yake kutuma ujumbe kupitia kwa wziri wa elimu kuwa hali yake ya kiafya siyo nzuri na hivyo kuahidi kuongea na makundi hayo hapo kesho.

Hali kwasasa bado siyo nzuri sana chuoni hapo kwani kila mmoja angali akiwa na shauku kujua nini Mh.waziri atasema hiyo kesho.
Imeletwa na mwakilishi wa blog hii UDOM
 (D.M)

No comments: