To Advertise on this Blog please Call: +255 (0)656 56 13 14 or Email: maishablog@yahoo.com                                                 To Advertise on this Blog please Call: +255 (0)656 56 13 14 or Email: maishablog@yahoo.com

Saturday 21 May 2011

Kumbukumbu miaka 15 ajari ya Mv Bukoba..


LEO ni Mei 21 siku ambayo Taifa linaingia kwenye kumbukumbu chungu ya kutimia miaka 15 tangu kutokea kwa ajali mbaya ya Mv Bukoba iliyochukua maisha ya Watanzania zaidi ya 300 waliokuwa wakisafiri kutoka Bukoba kuelekea jijini Mwanza.
Mara kadhaa watu wachache  walionusurika katika  ajali hiyo wamekuwa wakijitokeza kutoa ushuhuda wao jinsi mambo yalivyokuwa wakati  Meli hiyo ilipoinduka ikiwa inakaribia kuingia  Bandari  ya Mwanza.
Kitu cha  ajabu  ni kuwa  mpaka leo  serikali inaonekana bado iko usingizini katika  kuweka umakini  kwa vyombo vya usafiri nchini  jambo linalofanya  kuwepo kwa  ajali za  mara kwa mara  zinagharimu maisha ya  watanzania wengi  kwa uzembe wa watu wachache.
Siku za hivi karibuni tumekuwa tukishuhudia ajali mbaya za barabarani ambazo zimekuwa zikiacha historia na majonzi kwenye familia mbalimbali,pia kupoteza nguvu kazi ya taifa. Hivyo ni ombi na vilio vya wananchi kwa serikali, waendeshaji vyombo vya usafiri na wadau mabalimbali wa sekta hii kuwa makini katika kudhibiti aajari zisizo za lazima kutokea....
Mwisho naomba kuwapa pole wahanga wa ajari ya MV Bukoba na watanzania wote kwa ujumla mwenyezi Mungu awatie nguvu na kuwafariji.
toka G5

No comments: