To Advertise on this Blog please Call: +255 (0)656 56 13 14 or Email: maishablog@yahoo.com                                                 To Advertise on this Blog please Call: +255 (0)656 56 13 14 or Email: maishablog@yahoo.com

Thursday 25 August 2011

Kwa mara Nyingine tena "Anna Lukindo" afanya kweli kweli Uingereza!!!

 Jestina akiwa na mamodo wake tayari kwa kazi
 Jestina mwenyewe akiwajibika jukwaani
 Swala zima la make up likiendelea


 Pichani juu ni aina mbalimbali za mavazi yakiwa onyeshwa na mamodo
 Onyesho likiendelea
Pichani wadau waliokuja kutoa support kwenye onyesho hilo
Salam,



URBAN PULSE ikishirikiana na Miss Jestina Blog inakuletea matukio katika picha ya Mtanzania mbunifu wa kimataifa Anna Lukindo 
(anaetumia  jina la Anna Luks) alipoonyesha mavazi yake ya kibunifu mjini London. 
Maonyesho hayo ambayo yalifanyika Ijumaa tarehe 19 Agosti 2011 Chelsea Old Town Hall, King's Road, Chelsea London. SW3 5EE. 

Maonyesho hayo  yalienda sambamba na kusheherekea siku ya Ubinadamu duniani.

Anna ameonyesha ubunifu wake wa kipekee  wa kutumia vitambaa asilia mfano gunia, kamba za katani na nyuzi mbalimbali ambazo anatumia ufundi maalum na kutengeneza vitambaa vyake mwenyewe. Wadau kadhaa kutoka katika nyanja tofauti walijitokeza kwa wingi kumuunga mkono na kuvutiwa zaidi kwa  kazi zake. 
Maonyesho haya yalitayarishwa na Mdoe ambaye ni Mkurugenzi   Wa uchaguzi husika wa wasanii wenye vipaji vya maigizo jijini London. Mbali na shughuli nyingine za kidiplomasia yalikuwepo pia mashindano ya kutafuta mshindi wa Tuzo ya Uso wa mwaka 2012 yaliyoongozwa na mwonyeshaji urembo na mwanamichezo Rachel Christie. Baadaye yalifuatia maonyesho mawili ya mavazi "back to back" yaliyofanywa na wabunifu wawili wa mitindo Anna Lukindo wa Anna Luks na "Adopted Culture" msanifu wa rangi, Nana Antwi.


Kwa mawasiliano zaidi wasiliana na Anna kwa kutembelea tovuti yake hapo chini
http://annaluks.blogspot.com/
Twitter:@AnnaLukindo
ASANTENI,URBAN PULSE CREATIVE Akishirikiana na Miss Jestina Blog


No comments: